Wednesday, March 06, 2013

Kibanda aumizwa kama Dk. Ulimboka

Mhariri Mtendaji Mkuu wa New Habari, ambaye hadi Desemba 2012 alikuwa Mhariri Mtendaji wa Free Media, Absalom Kibanda, amevamiwa mbele ya lango la nyumba yake, Mbezi Beach, Dar es Salaam,  wakati anarejea kutoka kazini usiku; akapigwa; akang'olewa baadhi ya meno na kucha; akakatwa kidole na kuchomwa jicho. Kwa msaada wa watu mbalimbali, amesafirishwa kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu. Tunafuatilia maendeleo ya matibabu yake.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'