Chaguo Langu Mwaka Huu
Thursday, July 09, 2009
Saturday, July 04, 2009
Mahakama ya Kadhi: Ahadi nzito iliyoshindikana
IWAPO hoja ya Mahakama ya Kadhi Mkuu itafika mahali pa kuwakosanisha na kuwagombanisha Waislamu na Wakristo wa Tanzania, mgogoro huo utakuwa umesababishwa na woga wa watawala wetu. Kwa vipi? Soma Maswali Magumu wiki hii.
Sarah Palin abwaga manyanga

Sarah Palin, aliyekuwa mgombea mwenza wa John McCain kutoka chama cha Republican, Marekani, ametangaza kustaafu wadhifa wa Meya wa Alaska mwezi huu. Pata habari yenyewe.
Sunday, June 28, 2009
Michael Jackson: Skendo Tupu

Tumesikia na kusoma mengi mazuri ya Mfalme wa Pop, hayati Michael Jackson. Hapa kuna skendo za maisha yake ya nyumbani - yeye na pesa, watoto, ndugu, marafiki na majirani - zinazosimuliwa na mlezi wa watoto wake, Grace. Soma mwenyewe hapa.
Saturday, June 27, 2009
Serikali inataka kulikoroga jeshi letu?

Serikali imeamua kulipaka jeshi letu matope ya ufisadi, kulifanya ngao ya ufisadi wa vigogo, huku ikisisitiza kwamba ni kwa maslahi na usalama wa taifa. Je, inajua madhara yake? Ni haki kulitumia jeshi letu kulinda matumbo machafu ya wanasiasa? Huu ndio mjadala wa Maswali Magumu wiki hii.
Wednesday, June 24, 2009
Ijue Nguvu ya Sikio lako la Kulia
Ijue nguvu ya sikio lako na kulia na jinsi ya kulitumia la mwenzio katika mawasiliano. Soma hapa.
Tuesday, June 23, 2009
Uingereza wapata Spika mpinzani
Baada ya Spika wa awali kujiuzulu kwa kashfa, Bunge la Uingereza limechagua Spika mpya John Bercow (46) ambaye anatoka chama cha upinzani cha Conservative. Mtazame hapa akitambulishwa na kutambuliwa rasmi baada ya kupata baraka za Malkia; na hapa akikubali majukumu ya kazi yake mpya n akuwashukuru wabunge. Hizi hapa ni hotuba za viongozi wa vyama vikuu Bungeni: 1. Waziri Mkuu , Gordon Brown (Labour). 2. Kiongozi wa Upinzani , David Cameron (Conservative). 3. Kiongozi wa chama cha upinzani , Nick Clegg( Lib Dem). Msikilize Spika mpya akimnanga mbunge mzee aliyekataa kumuunga mkono kwa kigezo cha umri. Huu ndiyo utaratibu wa kumpata Spika wao.
Sunday, June 21, 2009
Rostam Mbunge Bubu

Imedhihirika kwamba miongoni mwa wabunge wote (319) wa Tanzania yupo mmoja, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (pichani kulia), ambaye hajawahi kuuliza swali Bungeni wala kuchangia katika mjadala wa jambo lolote katika vikao vya Bunge kwa zaidi ya miaka mitatu mfululizo (Desemba 2005-Juni 2009. ) Je, anatumia ubunge wake kufanya nini? Pitia orodha ya wabunge bubu wa Tanzania, utoe maoni yako.
Subscribe to:
Posts (Atom)
